Dira, Dhima, Lengo na Tunu

Dira

Kuwa Tume ya mfano katika utatuzi wa migogoro ya kikazi Afrika Mashariki.

Dhima

Kuhimiza mazingira ya amani eneo la kazi kupitia usuluhishi na uamuzi kuimarisha uzalishaji nchini.

Lengo

Lengo kuu la Tume ya Usuluhishi na Uamuzi ni kujenga ,kuimarisha na kukuza mahusiano bora na haki miongoni mwa waajiri na wafanyakazi Tanzania.

Tunu za msingi

Katika utekelezaji wa majukumu yake Tume itaongozwa na tunu za msingi zifutatazo:-

Uadilifu

Watumishi wetu watatekeleza majukumu yao kwa uaminifu na kwa haki bila kutoa au kupokea rushwa ya aina yoyote katika kipindi chote cha utekelezaji wa majukumu yao. Hawatatumia rasilimali za uma kwa manufaa binafsi.

Utaalamu

Watumishi wetu watazingatia utendaji bora katika maadili ya kitaalam.

Utendaji wa pamoja

Watumishi watazingatia utendaji wa pamoja ili kuhakikisha utoaji bora wa huduma. Kutakuwa na mawasiliano ya nyanja zote ya uhakika.

Uwajibikaji

Watumishi watawajibika kwa matendo yao katika utekelezaji wa majukumu ya Tume.

Uungwana na Utu

Watumishi watawahudumia wateja na wadau kwa uungwana , utu na heshima kwa msingi wa kujiheshimu na kuheshimu wengine

Huduma kwa wateja

Watumishi watatoa huduma kwa usawa na kwa wakati. Huduma itatolewa kwa uwazi kwa wateja wote.