Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Ridhiwani Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wakuu wa Taasisi mbalimbali mara baada ya maadhimisho ya Wiki ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Singida Aprili 28,2025.
Kauli Mbiu ya Maadhimisho hayo ni; "Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali Katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahali Pa Kazi".